TIGblogs TIG | TIGblogs GROUP TIGBLOGS LOGIN SIGNUP
TUSEME KISWAHILI


Tumearifiwa kwamba kunalo kundi la wanaTIG wanaoshughulikia tafsiri ya Kiswahili ya tovuti nzima. Tukiyangojea matokeo ya kazi yao kwa hamu, tumeamua kuunda ukumbi huu ili kuwapa wasemaji wa Kiswahili fursa kujadiliana, kuchangia fikra zao na kujieleza katika Kiswahili. Nia yetu ni kuwaunganisha wanaTIG ambao, vinginevyo, hawangeweza kuwasiliana. Tuyavunje mapingamizi yanayotuzuia, na baadaye tutaweza kuiendeleza na kuitukuza lugha yetu . Tunakaribisha maandishi ya aina yoyote: Visa vifupi, makala, madondo kutoka shajarani zenu nk. Ombi letu ni moja tu: tafadhali changieni katika Kiswahili.


Word on the street is that members of a TIG group are working on translating the website so that it will eventually be available in Kiswahili. In the meantime, this is a forum for all speakers of Kiswahili to exchange ideas and to express themselves in Kiswahili. We would like to build bridges connecting TIGers from different communities who may otherwise not be able to communicate with each other. Let us break down the barriers holding us back so that we may develop and promote our language. Stories, journal entries, poetry and any other writing are welcome. All that we ask is that you express yourself primarily in Kiswahili.



« previous 5


Nekesa   Nekesa Terri's TIGblog
Terri's profile

NI HUKUMU YA MUNGU AMA NI NINI HASWA?
Related to country: Kenya
About the book: "Think Big"


Hivi karibuni kumekuwa na mitetemeko ya ardhi ambayo imetishia uwezekano kwa kuongezeka kwa baa la njaa hapo duniani. Katika nchi ya Uchina, ambayo itakuwa inai…….michezo ya olimpiki mwaka huu, mitetemeko hii imekuwa moja baada ya nyingine. Jambo ambalo laweza kuongezea idhadi ya nchi ambazo hazitashiriki katika michezo hii. Si tu kwasababu ya mitetemeko hii bali juu ya mambo ya kisiasa yanayoendelea kati ya nchi ya Unchi na Tibeti.
Hapa nchini Kenya pia twaarifiwa ya kuwa milima kumi na tani ambayo iko katika bonde la ufa, ina uwezekano ya kulipuka saa yoyote ile. Ni dhairi shairi kwamba Mlima kama Kenya ambao haujadhibitishwa bado kama una uwezo wa kulipuka. Habari hizi zimetwaliwa kulingana na wanasayansi wa Kigiografia kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi. Pia haijulikani kama milima kama Elgon iliyodhibitishwa haiwezi tena kamwe kufanya hivyo?
Jambo la kusikitisha ni kwamba nchi ya Kenya haijatilia maanani mawaidha ya wabageografia hawa ya kuweka vidhibiti katika ardhi ili kuichunguza kwa umakini mitetemeko hii. Vidhibit hivi vinagharimu karibu shilingi milioni tano tu na vyaweza kuinusuru nchi yetu na nchi zingine ambazo zategema Kenya kama Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia na hata Sudan.
Katika sekta ya ukulima pia ambayo ndio kufanyika sana katika Bonde hili la ufa, maafa yaweza kuwa zaidi ya yale tunatarajia. Bonde la ufa ndilo lililo na idadi kubwa zaidi ya watu nchini kwa hivyo kukaweza kutukia milipuko hii, twaweza kupoteza halaiki kubwa sana ya watu! Pia twajua ya kuwa sehemu hii ndio inayokuza chakula kingi cha kulisha nchi nzima! Hivyo basi tukiangalia pande zote mbili, tutawapoteza watu walio na nguvu za luendeza uchumi wetu na pia kupoteza nafaka ambayo nchi nzima inatarajia kutumia kama chakula!
Serikali lazima ijue ya kwamba ina jukumu kubwa la kuwakidhi, kuwalinda na kuheshimu maisha ya wananchi wao na sit u porojo za siasa kila mara! Ni muhimu serikali yetu kuweza kuweka chini mipango ya kuviweka vidhiti hivi ili kuikoa nchi yetu kutokana na janga hili linalotunin’ginia!
Lakini, ni Mungu ambaye antuhukumu ama nini twaweza kujiuliza? Lazima tuchunguze mienendo yetu ingawa tutaweza kuishi bila vvikwazo hivi amabvyo vimetusoga hivi karibuni.

May 22, 2008 | 4:58 AM Comments  0 comments

Tags:


Terri   Terri Terri-Ann Gilbert-Roberts's TIGblog
Terri-Ann Gilbert-Roberts's profile

Siku iliyopita ...

Siku iliyopita niliwaza na kuwazua juu ya walioathirika na kupoteza makao yao walivyojipata katika janga hili la ufukura usiooleweka hadi sasa! Mawazo haya yote yalinijia nikiwa nikishiriki misa kaninsani, na si ya kuwa misa hiyo ilikuwa si ya kufana la hasha, lakini mambo niliyoshuhudia yalinifanya kushikwa na ghababu kuu sana!
Tulipofika kanisani misa ilikuwa ishaanza na kwa hivyo hatukuwa na budi kujitetea kwa kwenda kujaribu kumshawishi mwalimu wa dini kutupa benchi moja ili tuweze kuitumia humo kanisani. Pengine bahati yetu kwasababu tuliweza kuwapata Vijana wavulana wawili waliotusaidia kubeba benchi ile. Mara tulipofika kanisani, kundi kubwa la watu lilivamia benchi hiyo na kukaa ikabidi mmoja wa Vijana hao kukosa hata nafasi ya kuweza kujisitiri! Lahaula, waliosema usistaajabu ya musa ya firauni hujayaona kweli alinena. Nilibaki mdomo wazi kwa vile sikuweza kufikiri ya kuwa jambo kama hilo lingeliweza kutendeka katika hadhara na kwa kusitiza hii iliyo na wakristo wanaomcha Mungu! Nilifunzwa tangu utotoni kumpa mtu yeyote haki yake na moja ya haki hizi kulingana name ni kumpa nafasi mtu aliyebeba benchi hiyo nafasi ya kwanza na ilkiwa itakuwa ipo bado basi wengine nao wafuate kuanzia wakubwazo!

Nilishangaa na kwa kuwa sikutaka kuonekana kuwa alipigwa na butwaa, mawazo mengi sana yalinijia na nikaweza kulinganisha yaliyotendeka na vile wahasiriwa waliopoteza makao yao yalivyonijia!

Jamani wenzangu twaweza kuishi maisha yasiokuwa na kuwanyang’anya wenzetu yaliyo yao ya haki??

April 2, 2008 | 6:04 AM Comments  0 comments

Tags:


Nekesa   Nekesa Terri's TIGblog
Terri's profile

Siku iliyopita ...

Siku iliyopita niliwaza na kuwazua juu ya walioathirika na kupoteza makao yao walivyojipata katika janga hili la ufukura usiooleweka hadi sasa! Mawazo haya yote yalinijia nikiwa nikishiriki misa kaninsani, na si ya kuwa misa hiyo ilikuwa si ya kufana la hasha, lakini mambo niliyoshuhudia yalinifanya kushikwa na ghababu kuu sana!
Tulipofika kanisani misa ilikuwa ishaanza na kwa hivyo hatukuwa na budi kujitetea kwa kwenda kujaribu kumshawishi mwalimu wa dini kutupa benchi moja ili tuweze kuitumia humo kanisani. Pengine bahati yetu kwasababu tuliweza kuwapata Vijana wavulana wawili waliotusaidia kubeba benchi ile. Mara tulipofika kanisani, kundi kubwa la watu lilivamia benchi hiyo na kukaa ikabidi mmoja wa Vijana hao kukosa hata nafasi ya kuweza kujisitiri! Lahaula, waliosema usistaajabu ya musa ya firauni hujayaona kweli alinena. Nilibaki mdomo wazi kwa vile sikuweza kufikiri ya kuwa jambo kama hilo lingeliweza kutendeka katika hadhara na kwa kusitiza hii iliyo na wakristo wanaomcha Mungu! Nilifunzwa tangu utotoni kumpa mtu yeyote haki yake na moja ya haki hizi kulingana name ni kumpa nafasi mtu aliyebeba benchi hiyo nafasi ya kwanza na ilkiwa itakuwa ipo bado basi wengine nao wafuate kuanzia wakubwazo!

Nilishangaa na kwa kuwa sikutaka kuonekana kuwa alipigwa na butwaa, mawazo mengi sana yalinijia na nikaweza kulinganisha yaliyotendeka na vile wahasiriwa waliopoteza makao yao yalivyonijia!

Jamani wenzangu twaweza kuishi maisha yasiokuwa na kuwanyang’anya wenzetu yaliyo yao ya haki??

April 2, 2008 | 6:04 AM Comments  0 comments

Tags:


Terri   Terri Terri-Ann Gilbert-Roberts's TIGblog
Terri-Ann Gilbert-Roberts's profile

Ni vema kabisa ...

Ni vema kabisa kuelewa swala au mswaada wa mambo yanavyo endela nchini Kenya.Hivi tunavyozungumza, sheria mbili mwafaka za kuidhinisha ofisi ya Waziri mkuu na pia tume ya kuchunguza na kuhakikisha ukweli na haki zimeshatiwa sahihi na sasa zangojea tu kuandikishwa rasmi .
Twaona kwamba pia wanasiasa wameweza kuyaweka masilahi ya wakenya kwanza na kwa moyo wote kuunga mkono miswaada hii. Katika bunge, twaona ya kuwa Rais Kibaki alihudumu kikao hiki cha tatu kama Mbunge wa Othaya na wala si kama rais. Hii ni dhairi shairi kwamba pia yeye ameunga mikakati inayo endelea ya kuwezesha amani nchini Kenya. Chama cha ODM ambacho kilionekana kuweza kuanza kuwa na migogoro hivi karibuni , kupitia kwa msimamo ambao Kigogo wa Pentagon bwana Ruto aliokuwa ameuchukuwa, kimefikia maelewano ambayo yameleta utulivu. Bwana Ruto ametangaza hadharani kuwa anaunga mkono kuteuliwa kwa Bwana Musalia Mudavadi kama Naibu wa waziri mkuu. Bwana Ruto alitangaza haya akiwa katika eneo lake la bunge la allipohodhuria sherehe ya kuwatuza wanafunzi bora katika shule ya wanafunzi ya wasichna ya Eldoret.Musalia Mudavadi anayejulikana kwa umaarfufu kama ‘Double M’ , ni mbunge wa Sabatia katika mkoa wa Magharibi.

Twaomba kama wakenya na hasa wana TIG ya kuwa miswaada iliyoutiwa sahihi, itafuata kwa makini na kila anayehusika atatia for a na kufanya jukumu lake la kuhakikisha ya kuwa mambo yaliyojadiliwa yatatimizwa.

March 20, 2008 | 11:03 AM Comments  0 comments

Tags:


Nekesa   Nekesa Terri's TIGblog
Terri's profile

Ni vema kabisa ...

Ni vema kabisa kuelewa swala au mswaada wa mambo yanavyo endela nchini Kenya.Hivi tunavyozungumza, sheria mbili mwafaka za kuidhinisha ofisi ya Waziri mkuu na pia tume ya kuchunguza na kuhakikisha ukweli na haki zimeshatiwa sahihi na sasa zangojea tu kuandikishwa rasmi .
Twaona kwamba pia wanasiasa wameweza kuyaweka masilahi ya wakenya kwanza na kwa moyo wote kuunga mkono miswaada hii. Katika bunge, twaona ya kuwa Rais Kibaki alihudumu kikao hiki cha tatu kama Mbunge wa Othaya na wala si kama rais. Hii ni dhairi shairi kwamba pia yeye ameunga mikakati inayo endelea ya kuwezesha amani nchini Kenya. Chama cha ODM ambacho kilionekana kuweza kuanza kuwa na migogoro hivi karibuni , kupitia kwa msimamo ambao Kigogo wa Pentagon bwana Ruto aliokuwa ameuchukuwa, kimefikia maelewano ambayo yameleta utulivu. Bwana Ruto ametangaza hadharani kuwa anaunga mkono kuteuliwa kwa Bwana Musalia Mudavadi kama Naibu wa waziri mkuu. Bwana Ruto alitangaza haya akiwa katika eneo lake la bunge la allipohodhuria sherehe ya kuwatuza wanafunzi bora katika shule ya wanafunzi ya wasichna ya Eldoret.Musalia Mudavadi anayejulikana kwa umaarfufu kama ‘Double M’ , ni mbunge wa Sabatia katika mkoa wa Magharibi.

Twaomba kama wakenya na hasa wana TIG ya kuwa miswaada iliyoutiwa sahihi, itafuata kwa makini na kila anayehusika atatia for a na kufanya jukumu lake la kuhakikisha ya kuwa mambo yaliyojadiliwa yatatimizwa.

March 20, 2008 | 11:03 AM Comments  0 comments

Tags:


« previous 5


Owner
This Group TIGBlog is owned by: R Oburra.

Membership
Miguel
Christabell
Connie Wokuri
NKATHA
judy
Maxence M. Melo
David Diogène
Norma
Kahendi
Rahab
Terri
Terri-Ann Gilbert-Roberts
VICTOR RASUGU
Vitalis Wafula Wekesa

You must be logged in to join this group TIGblog.

Latest Posts
NI HUKUMU YA MUNGU AMA...
Siku iliyopita ...
Siku iliyopita ...
Ni vema kabisa ...
Ni vema kabisa ...

Monthly Archive
December 2007
January 2008
February 2008
March 2008
April 2008
May 2008

Change Language



3199 views
Important Disclaimer