Siku iliyopita niliwaza na kuwazua juu ya walioathirika na kupoteza makao yao walivyojipata katika janga hili la ufukura usiooleweka hadi sasa! Mawazo haya yote yalinijia nikiwa nikishiriki misa kaninsani, na si ya kuwa misa hiyo ilikuwa si ya kufana la hasha, lakini mambo niliyoshuhudia yalinifanya kushikwa na ghababu kuu sana!
Tulipofika kanisani misa ilikuwa ishaanza na kwa hivyo hatukuwa na budi kujitetea kwa kwenda kujaribu kumshawishi mwalimu wa dini kutupa benchi moja ili tuweze kuitumia humo kanisani. Pengine bahati yetu kwasababu tuliweza kuwapata Vijana wavulana wawili waliotusaidia kubeba benchi ile. Mara tulipofika kanisani, kundi kubwa la watu lilivamia benchi hiyo na kukaa ikabidi mmoja wa Vijana hao kukosa hata nafasi ya kuweza kujisitiri! Lahaula, waliosema usistaajabu ya musa ya firauni hujayaona kweli alinena. Nilibaki mdomo wazi kwa vile sikuweza kufikiri ya kuwa jambo kama hilo lingeliweza kutendeka katika hadhara na kwa kusitiza hii iliyo na wakristo wanaomcha Mungu! Nilifunzwa tangu utotoni kumpa mtu yeyote haki yake na moja ya haki hizi kulingana name ni kumpa nafasi mtu aliyebeba benchi hiyo nafasi ya kwanza na ilkiwa itakuwa ipo bado basi wengine nao wafuate kuanzia wakubwazo!
Nilishangaa na kwa kuwa sikutaka kuonekana kuwa alipigwa na butwaa, mawazo mengi sana yalinijia na nikaweza kulinganisha yaliyotendeka na vile wahasiriwa waliopoteza makao yao yalivyonijia!
Jamani wenzangu twaweza kuishi maisha yasiokuwa na kuwanyang’anya wenzetu yaliyo yao ya haki??