TIGblogs TIG | TIGblogs GROUP TIGBLOGS LOGIN SIGNUP
TUSEME KISWAHILI
Tumearifiwa kwamba kunalo kundi la wanaTIG wanaoshughulikia tafsiri ya Kiswahili ya tovuti nzima. Tukiyangojea matokeo ya kazi yao kwa hamu, tumeamua kuunda ukumbi huu ili kuwapa wasemaji wa Kiswahili fursa kujadiliana, kuchangia fikra zao na kujieleza katika Kiswahili. Nia yetu ni kuwaunganisha wanaTIG ambao, vinginevyo, hawangeweza kuwasiliana. Tuyavunje mapingamizi yanayotuzuia, na baadaye tutaweza kuiendeleza na kuitukuza lugha yetu . Tunakaribisha maandishi ya aina yoyote: Visa vifupi, makala, madondo kutoka shajarani zenu nk. Ombi letu ni moja tu: tafadhali changieni katika Kiswahili.


Word on the street is that members of a TIG group are working on translating the website so that it will eventually be available in Kiswahili. In the meantime, this is a forum for all speakers of Kiswahili to exchange ideas and to express themselves in Kiswahili. We would like to build bridges connecting TIGers from different communities who may otherwise not be able to communicate with each other. Let us break down the barriers holding us back so that we may develop and promote our language. Stories, journal entries, poetry and any other writing are welcome. All that we ask is that you express yourself primarily in Kiswahili.



Terri   Terri Terri-Ann Gilbert-Roberts's TIGblog
Terri-Ann Gilbert-Roberts's profile

Ni vema kabisa ...

Ni vema kabisa kuelewa swala au mswaada wa mambo yanavyo endela nchini Kenya.Hivi tunavyozungumza, sheria mbili mwafaka za kuidhinisha ofisi ya Waziri mkuu na pia tume ya kuchunguza na kuhakikisha ukweli na haki zimeshatiwa sahihi na sasa zangojea tu kuandikishwa rasmi .

Twaona kwamba pia wanasiasa wameweza kuyaweka masilahi ya wakenya kwanza na kwa moyo wote kuunga mkono miswaada hii. Katika bunge, twaona ya kuwa Rais Kibaki alihudumu kikao hiki cha tatu kama Mbunge wa Othaya na wala si kama rais. Hii ni dhairi shairi kwamba pia yeye ameunga mikakati inayo endelea ya kuwezesha amani nchini Kenya. Chama cha ODM ambacho kilionekana kuweza kuanza kuwa na migogoro hivi karibuni , kupitia kwa msimamo ambao Kigogo wa Pentagon bwana Ruto aliokuwa ameuchukuwa, kimefikia maelewano ambayo yameleta utulivu. Bwana Ruto ametangaza hadharani kuwa anaunga mkono kuteuliwa kwa Bwana Musalia Mudavadi kama Naibu wa waziri mkuu. Bwana Ruto alitangaza haya akiwa katika eneo lake la bunge la allipohodhuria sherehe ya kuwatuza wanafunzi bora katika shule ya wanafunzi ya wasichna ya Eldoret.Musalia Mudavadi anayejulikana kwa umaarfufu kama ‘Double M’ , ni mbunge wa Sabatia katika mkoa wa Magharibi.



Twaomba kama wakenya na hasa wana TIG ya kuwa miswaada iliyoutiwa sahihi, itafuata kwa makini na kila anayehusika atatia for a na kufanya jukumu lake la kuhakikisha ya kuwa mambo yaliyojadiliwa yatatimizwa.

March 20, 2008 | 11:03 AM Comments  2 comments

Tags:
You must be logged in to add tags.


Comments

nsetak ahmed
April 23, 2010 | 10:21 AM

thank u my dear

مصر العاب العاب بنات العاب بنات جديدة
smalltoto ahmed saeed
September 17, 2011 | 9:19 AM

thannx

العاب فلاش بنات سيارات طبخ الروقان :D
http://games.rwa2an.org
http://dolls-games.rwa2an.org
http://racing.rwa2an.org
http://cooking.rwa2an.org
http://dolls-games.rwa2an.org/Dolls-Cat1
http://flash-games.trq3a.com
http://www.rwa2an.net/vb
http://banat-games.trq3a.com
http://www.bakaar.com
http://www.dorragames.com
Owner
This Group TIGBlog is owned by: R Kahendi.

Membership
You must be logged in to join this group TIGblog.

Latest Posts
Utapiamlo (Malnutrition)
NI HUKUMU YA MUNGU AMA...
Siku iliyopita ...
Siku iliyopita ...
Ni vema kabisa ...

Monthly Archive
January 2008
March 2008
April 2008
May 2008
July 2008

Change Language



14845 views
Important Disclaimer