Hivi karibuni kumekuwa na mitetemeko ya ardhi ambayo imetishia uwezekano kwa kuongezeka kwa baa la njaa hapo duniani. Katika nchi ya Uchina, ambayo itakuwa inai…….michezo ya olimpiki mwaka huu, mitetemeko hii imekuwa moja baada ya nyingine. Jambo ambalo laweza kuongezea idhadi ya nchi ambazo hazitashiriki katika michezo hii. Si tu kwasababu ya mitetemeko hii bali juu ya mambo ya kisiasa yanayoendelea kati ya nchi ya Unchi na Tibeti.
Hapa nchini Kenya pia twaarifiwa ya kuwa milima kumi na tani ambayo iko katika bonde la ufa, ina uwezekano ya kulipuka saa yoyote ile. Ni dhairi shairi kwamba Mlima kama Kenya ambao haujadhibitishwa bado kama una uwezo wa kulipuka. Habari hizi zimetwaliwa kulingana na wanasayansi wa Kigiografia kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi. Pia haijulikani kama milima kama Elgon iliyodhibitishwa haiwezi tena kamwe kufanya hivyo?
Jambo la kusikitisha ni kwamba nchi ya Kenya haijatilia maanani mawaidha ya wabageografia hawa ya kuweka vidhibiti katika ardhi ili kuichunguza kwa umakini mitetemeko hii. Vidhibit hivi vinagharimu karibu shilingi milioni tano tu na vyaweza kuinusuru nchi yetu na nchi zingine ambazo zategema Kenya kama Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia na hata Sudan.
Katika sekta ya ukulima pia ambayo ndio kufanyika sana katika Bonde hili la ufa, maafa yaweza kuwa zaidi ya yale tunatarajia. Bonde la ufa ndilo lililo na idadi kubwa zaidi ya watu nchini kwa hivyo kukaweza kutukia milipuko hii, twaweza kupoteza halaiki kubwa sana ya watu! Pia twajua ya kuwa sehemu hii ndio inayokuza chakula kingi cha kulisha nchi nzima! Hivyo basi tukiangalia pande zote mbili, tutawapoteza watu walio na nguvu za luendeza uchumi wetu na pia kupoteza nafaka ambayo nchi nzima inatarajia kutumia kama chakula!
Serikali lazima ijue ya kwamba ina jukumu kubwa la kuwakidhi, kuwalinda na kuheshimu maisha ya wananchi wao na sit u porojo za siasa kila mara! Ni muhimu serikali yetu kuweza kuweka chini mipango ya kuviweka vidhiti hivi ili kuikoa nchi yetu kutokana na janga hili linalotunin’ginia!
Lakini, ni Mungu ambaye antuhukumu ama nini twaweza kujiuliza? Lazima tuchunguze mienendo yetu ingawa tutaweza kuishi bila vvikwazo hivi amabvyo vimetusoga hivi karibuni.